Kwa mujibu wa mwandishi wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatullah Sayyid Hashim Husseini Bushehri, katika khutuba za Swala ya Ijumaa ya tarehe 20 Shahrivar 1405 mjini Qom, iliyofanyika ndani ya Muswalla wa Quds, amesema: “Ushiriki mkubwa wa wananchi katika shughuli za mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi ulikuwa ishara ya mapenzi na upendo wa wananchi wa Iran na Iraq kwake. Na kwa heshima ya mapenzi waliyomuonesha kiongozi shahidi wa Mapinduzi, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi pia alituma ujumbe maalumu ili kuwashukuru viongozi wa Iraq, waendeshaji wa Mawakibu, pamoja na makabila na koo, lakini wao walisema: ‘Hili lilikuwa ni jukumu letu.’”
Imam wa Ijumaa wa Qom amesema: “Watu wote wanaopenda Wilaya katika maeneo mbalimbali duniani walionesha mapenzi yao kwa kiongozi shahidi wa Mapinduzi, na kama kungekuwa hakuna vikwazo vya maadui katika nchi zinazotuchukia, jambo kubwa sana lingetokea.”
Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Wataalamu wa Uongozi ameongeza: “Wananchi wamekuwa katika uwanja wa mapambano na mitaani kwa zaidi ya usiku 190, kwa mujibu wa kauli ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi kwamba watu watahamasika na kujitokeza. Kama alivyosema Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi, katika kipindi kati ya kuuawa kishahidi kiongozi huyo na hadi kufanyika uchaguzi wa kihistoria wa Baraza la Wataalamu wa Uongozi, wananchi walichukua jukumu la uongozi na kudhibiti mitaa ili adui asiweze kupenya.”
Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Qom amesisitiza: “Tuijue thamani ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi. Maadui wanaeneza propaganda nyingi za uongo, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi anazisifu huduma za Serikali na kusisitiza kwamba tunapaswa kutaja maeneo yenye nguvu, tunapokuwa na adui na kutaja udhaifu wetu kunaweza kumpa adui fursa ya kututumia vibaya, basi ukosoaji haupaswi kutolewa katika anga ya umma, kauli hizi tunapaswa kuzithamini na kuzichukulia kama mtaji muhimu.”
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Qom amerejea sababu zilizopelekea kuanza kwa vita vilivyolazimishwa dhidi ya Iran na kusema: “Netanyahu, ambaye ni adui wa Uislamu na Mapinduzi ya Kiislamu, alimchochea Trump kwamba pande zinazozunguka Iran zimeshindwa na mabawa ya Iran yamevunjwa; kwa hiyo, sasa ni fursa nzuri ya kuipiga Serikali pigo kubwa na kuipindua.”
Ayatullah Hussini Bushehri aliendelea kusema: “Walidhani kwamba kwa kuuawa kishahidi kiongozi wa Mapinduzi na makamanda wa kijeshi tutashindwa, lakini taifa hili liliposikia habari za kuuawa kishahidi kiongozi wa Mapinduzi, wakati jua lilikuwa bado halijachomoza, lilijitokeza mitaani na bado liko mitaani.”
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Qom ameendelea kusema: “Taifa hili halitaanguka mbele ya njama za Ikulu ya White House, kwa sababu lina hamasa ya kidini na limesimama imara katika uwanja huu.”
Imam wa Ijumaa wa Qom amesema: “Leo watu wa Marekani wanawauliza viongozi wao: Kwa nini mmetupeleka katika shimo ambalo hatuwezi kutoka? Hawajui kwamba watu wa Iran ni kizazi cha wale waliomwambia Imam Hussein (as): ‘Hata tukiuawa maelfu ya mara, bado tutapigana tukiwa pamoja nawe.’ Kwa sababu hiyo, wamefanya makosa katika tathmini zao.”
Akizungumzia kuangushwa kwa makombora maalumu na manowari za Marekani, amesema: “Baadhi ya watu ndani ya nchi walikuwa na matumaini kwamba iwapo tungefanya mazungumzo, tungefikia matokeo. Kiongozi shahidi wa Mapinduzi alikuwa ameshauri mara kadhaa kutumia uzoefu katika njia hii lakini wao walitushambulia wakati wa mazungumzo na wakavunja mikataba yao.”
Ayatullah Husseini Bushehri amesisitiza: “Hadi sasa tumefanya mazungumzo kwa ajili ya kuwashawishi wananchi na wale waliokuwa na matumaini katika mazungumzo. Sisi si watu wa vita, lakini katika vita tulivyolazimishiwa hatutarudi nyuma, na kwa mujibu wa makamanda wetu, ikiwa mtalenga shabaha mbili, sisi tutalenga shabaha 20.”
Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Qom amesema: “Leo dunia nzima inaitania Marekani kutokana na kupoteza ndege aina ya F-35 na manowari. Kwa baraka ya nguvu ya Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu, vikosi vya kijeshi na wananchi wa Iran, utawala wa nguvu wa Marekani umevunjwa, na mataifa mengine yenye nguvu yamepata utulivu.”
Ameongeza: “Msemaji wa taasisi ya diplomasia anaweza kusema kwamba leo sisi pia tuko katika kiwango cha nchi zenye nguvu na tunahesabiwa kuwa miongoni mwa mataifa yenye nguvu kubwa duniani, kama alivyosema kiongozi shahidi wa Mapinduzi, leo tunapaswa kuwa na nguvu zaidi kuliko wakati mwingine wowote.”
Ayatullah Husseini Bushehri ameongeza: “Mlingano wa kisiasa na kiuchumi wa adui umevurugika, bei ya mafuta inaendelea kupanda, na Trump ana kiwango cha chini zaidi cha umaarufu miongoni mwa marais wa Marekani, haya yametokea kutokana na uvumilivu na kusimama kwenu imara.”
Ameendelea kusema: “Kwa mujibu wa wataalamu, Warepublican wanapaswa kuondoka katika Baraza la Wawakilishi na Seneti. Sisi pia hatuna furaha na Democrats, lakini hawa wamekuja kupigana na Uislamu na Iran na wametufanya tuomboleze, kwa sababu hiyo, wanapaswa kuondoka, na bila shaka wataondoka katika uwanja huu wakiwa wamefedheheka.”
Imam wa Ijumaa wa Qom amesema: “Mlango wa Hormuz umegeuka kuwa jinamizi kwa adui, wanakiri kwamba kama Iran ingekuwa na bomu la atomiki, ingekuwa bora kuliko Iran kuufunga Mlango wa Hormuz. Kiongozi shahidi wa Mapinduzi alisema: ‘Ikiwa mtaendelea na vitendo vyenu vya kikatili, vita vitageuka kuwa vya kikanda.’ Kiongozi huyo shahidi hayupo tena ili aone kwamba vita vimevuka mipaka ya kikanda na kuwa vya kimataifa, na kwamba adui ameathirika hata katika maeneo ya mbali zaidi.”
Ayatullah Husseini Bushehri, huku akiwapongeza wapiganaji wa Yemen ambao ni marafiki wa kweli wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saww), amesema: “Kama vile Mlango wa Hormuz uko chini ya udhibiti wa Iran, vivyo hivyo Mlango wa Bab al-Mandab uko chini ya udhibiti wa wananchi wa Yemen.”
Khutibu wa Swala ya Ijumaa ya Qom ametaja kukwepa kulipa gharama kuwa sababu nyingine na kuongeza: “Ushindi haupatikani kwa urahisi. Watu wanapaswa kulipa gharama za kifedha, za maisha na hata za heshima kwa ajili yake, lakini baadhi ya watu hawako tayari kulipa gharama yoyote kwa ajili ya ushindi.”
Maoni yako